Showing posts with label NEWS. Show all posts
Showing posts with label NEWS. Show all posts

Monday, February 13, 2012

WHITNEY HOUSTON AFARIKI DUNIA AKIWA NA MIAKA 48

 Breaking News

Mwimbaji na muigizaji maarufu kutoka nchini Marekani,Whitney Houston,amefariki dunia muda mfupi uliopita(Jumamosi mchana saa tisa na dakika hamsini na tano kwa saa za Marekani-Pacific) akiwa na umri wa miaka 48. Whitney Houston ambaye ni miongoni mwa waimbaji waliokuwa na kipaji cha aina yake katika uimbaji,amekutwa na walinzi wake wa karibu(bodyguards) akiwa hajitambui katika gorofa ya nne ya chumba cha hotel ya The Beverly Hilton alipokuwa amefikia. Watu wa dharura walijaribu kuokoa maisha yake bila mafanikio na hivyo ikatangazwa rasmi kwamba amefariki.

Thursday, February 2, 2012

Profesa Mwandosya arudi India

*Dkt. Mwakyembe aonekana ofisini mara moja

WAZIRI wa Maji, Profesa Mark Mwandosya, ameondoka nchini juzi kwenda India
ili kuangalia maendeleo ya afya yake ambapo Naibu Waziri wa Ujenzi, Dkt. Harrison Mwakyembe, akidaiwa kuripoti ofisini mara moja tangu arejee nchini.

Maiti ya jambazi Arusha yazua 'kasheshe'


Ndugu wasusa mwili mochari, wachukuliwa na Mchungaji 

NDUGU wa jambazi sugu aliyeuawa na polisi Januari 13
mwaka huu, Bw. Pokea Kayaa (45), maarufu 'Steven Kaunda', wamesusa kuchukua maiti yake katika Hospitali ya Mount Meru, mjini Arusha.
Kutokana na hali hiyo, Mchungaji wa Kanisa la Tumaini Assemblies of God, wilayani Arumeru, Amani Silanga, akiwa na baadhi ya watu waliomfahamu Bw. Kaaya, walilazimika kwenda hospitali kuchukua mwili huo na kuusafirisha jijijini kwake Nkoanrua.


Labels